Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, March 14, 2014

WATU WANNE WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE BADO WAMENASA BAADA YA KIFUSI KUPOROMOKA KATIKA MACHIMBO YA DHAHABU

Watu wanne wamefariki dunia na wengine kadhaa bado wamenasa kwenye kifusi katika machimbo madogo ya Kalole kata ya Lunguya wilayani kahama mkoani Shinyanga kufuatia kuporomoka kwa duara waliyokuwa wanachimba Dhahabu.
Diwani wa Kata ya Lunguya Benedicto Manwari ameiambia Radio Kahama FM tukio hilo limetokea jana jioni, na kwamba hadi kufikia jioni hii miili ya watu wane imeopolewa na majeruhi mmoja ambaye anapatiwa matibabu katika kituo cha Afya Lunguya.


Manuari amesema miili mitatu ni wakazi wa hapo Kalole na mmoja ni wa kutoka Bariadi mkoani Simiyu ambapo tayari umekwishasafirishwa na kwamba Yule majeruhi ambaye amevunjika mkono na ana jeraha usoni ni mtu wa Morogoro.
Amesema kufuatia sensa iliyofanywa, inakisiwa watu watatu wakazi wa kijijini hapo bado wamenasa katika kifusi hicho ingawaji juhudi za uopoaji bado zinaendelea japokuwa hakuna msaada wowote wa zana za kisasa ulioweza kupatikana.
Manuari amesema Serikali ngazi ya wilaya imepewa taarifa hizo na Jeshi la Polisi limekwishafika kwenye eneo la tukio.
Balaa la watu kupoteza maisha katika machimbo madogo ya madini bado halijapata jibu la kudumu kwa wilaya ya Kahama ambayo imekuwa ikiibuka kugunduliwa madini karibu kila sehemu ya ardhi yake.

No comments:

Post a Comment