MAJANGA
BARCA!. Mshambuliaji wao raia wa Brazil, Neymar ataa nje ya uwanja wa
wiki nne, wakati naye beki Jordi Alba atakaa muda kama huo baada ya wote
kupata majeruhi.
Klabu
ya Barcelona imethibitisha kuwa Neymar alipata majeruhi ya mguu jana
katika mchezo wa fainali ya kombe la Mfalme dhidi ya Real Madrid.
Kinda
huyo mwenye miaka 21 alishindwa kuisaidia Barca kuepukana na kipigo cha
mabao 2-1, huku Mbrazil huyo akikosa nafasi ya wazi dakika za lala
salama.
Neymar atakosa mechi zijazo dhidi ya Athletic Bilbao, Villarreal, Getafe na Elche.
Hata hivyo klabu ya Barca ina matumaini kuwa nyota wake huyo anaweza kurudi katika mechi ya mwisho dhidi ya Atletico Madrid.Na Baraka Mpenja
No comments:
Post a Comment