Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, February 4, 2016

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AWASILI MKOANI SINGIDA KWA MAANDALIZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 39 YA CHAMA HICHO

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na  Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Vicent Kone mara baada kuwasili mkoani humo jioni ya leo,tayari kwa kuanza maandalizi ya shamra shamra za maadhimisho ya chama cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 39 Kitaifa mkoani Singida.Sherehe hizo zitakazofanyika Februari 6 2016 zinatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho.
Ndugu Kinana akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Said Amanzi baada ya kuwasili Singida leo,kulia kwake ni MKuu wa Mkoa wa Singida  Dk.Parseko Vicent Kone  

 
 Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Vicent Kone sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Singida Said Amanzi wakiwa na wageni wao ,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye mara baada kupokelewa jioni ya leo mjini humo
 Mwenyeki wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Singida Bi.Diana Chilolo  samba na Mkuu wa Mkoa Dk.Parseko Vicent Kone wakiwakaribisha wageni wao jioni ya leo mkoani humo.
Baadhi ya Wafuasi wa chama cha CCM wakijimwaya mwaya mara baada ya kuwapokea wageni wao waliowasili jioni ya leo mkoani humo.
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukiwasili mkoani Singida jioni ya leo kwa ajili ya maandalizi ya shamra shamra za maadhimisho ya chama cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 39 Kitaifa mkoani Singida,ambapo sherehe hizo ambazo zitahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho zinatarajiwa kurindima Februari 6 2016 katika uwanja wa Namfua.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya wafuasi wa chama hicho waliofika kumlaki mara baada ya kuwasili mkoani humo jioni ya leo,tayari kwa kuanza maandalizi ya shamra shamra za maadhimisho ya chama cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 39 Kitaifa mkoani Singida.Sherehe hizo zitakazofanyika Februari 6 2016 zinatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Mhe. Nape Nnauye akisalimiana na baadhi ya wafuasi wa chama hicho waliofika kuwalaki mara baada ya kuwasili mkoani humo jioni ya leo,tayari kwa kuanza maandalizi ya shamra shamra za maadhimisho ya chama cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 39 Kitaifa mkoani Singida.Sherehe hizo zitakazofanyika Februari 6 2016 zinatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama hicho.
 Mwenye wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Singida Bi.Diana Chilolo akimlaki Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa,Ndugu Nape Nnauye mara baada ya kuwasili mkoani humo akiwa ameambatana Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana tayari kwa maandalizi ya maadhimisho ya chama hicho kutimiza miaka 39,ambapo kilele chake itakuwa Februari 6 ndani uwanja wa Namfua.

No comments:

Post a Comment