Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, April 30, 2014

MIILI ASKARI WALIKUFA KATIKA AJALI YA SUMRY YASAFIRISHWA

Majeneza yenye miili ya askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani waliofariki dunia baada ya kugongwa na basi wakati wakipima ajali usiku wa kuamkia jana katika Kijiji cha Utaho, wilayani Ikungi, mkoa wa Singida kabla ya kuagwa na kusafirishwa.
Katika ajali hiyo pia watu 19 wa kijiji cha Utaho wilayani Ikungi wamepoteza maisha wakiwemo askari wanne wa jeshi la polisi, baada ya kugongwa na basi la Summry wakati wakiwa wana toa msaada wa kumpakia marehemu kwenye gari la polisi aliye gongwa na gari kubwa ambalo halikufahamika mara moja . Basi hilo la kampuni ya Sumry hufanya safari zake kati ya Kigoma na Dar-es-salaam.

No comments:

Post a Comment