Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, April 19, 2014

TAARIFA YA MELI ILIYOZAMA MWANZA

Watu 10 wamenusurika kufa maji katika ziwa 
Victoria baada ya meli ya mizigo Fb Matara 
kupinduka na kuzama ikiwa na shehena ya sukari 
tani 280 zilizonunuliwa katika kiwanda cha sukari 
Kagera wakati ikitoka Bukoba kwenda jijini

Mwanza
Meli hiyo inayomilikiwa na kampuni ya Mkombozi 
fishing and marine transport limited, imezama 
ikiwa na magunia 5600 ya sukari sawa na tani
280, mali ya mfanyabiashara wa jijini Mwanza
aitwaye V.h.Shah, ambapo mkurugenzi wa
kampuni hiyo Gitano Chacha Munanka ameeleza
kwamba meli hiyo imezama ikiwa katikati ya visiwa
vya Kerebe na Lukolu majira ya saa 10.30 usiku 
na kuongeza kwamba hakuna mtu yeyote
aliyejeruhiwa kufuatia tukio hilo.
ITV imeshuhudia meli hiyo ikiwa imepinduka huku
juhudi za wafanyakazi wa kampuni hiyo kuipundua
zikiwa zinaendelea bila mafanikiohuku baadhi ya
mashuhuda wa tukio hilo wakisema chanzo cha
meli hiyo kuzama ni kutokana na dhoruba kali
ambapo wametoa ushauri kwa wamiliki wa vyombo
vya majini kuzingatia utabiri unaotolewa na
mamlaka ya hali ya hewa nchini ili kuepusha
maafa.
Meli hii inayoonekana pichani ni mfano wa meli
iliyozama,ambayo ilianza safari yake ya kutoka
Bukoba majira ya saa 7 mchanaikiwa
inaendeshwa na kapteni Erick Lasana – mamlaka
ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu
Sumatra kanda ya ziwaumethibitisha kuzama kwa
meli hiyo yenye uwezo wa kubeba tani 280 za
mizigo na abiria 100.
>>>>>>>>>chanzo ITV

No comments:

Post a Comment