Pata hiyo na ukome: Shabiki wa Liverpool akimchapa konde wa Chelsea nje ya Uwanja wa Anfield
VURUGU ilizotokea nje ya Uwanja wa Anfield kufuatia Liverpool kufungwa na Chelsea mabao 2-0 jana.
Picha zinaonyesha kitimutimu cha maana nje ya Uwanja wa Anfield Road baada ya mashabiki wa Liverpool kuwavaa mashabiki wa Chelsea waliokuwa wakiimba jina la Nahodha wa Wekundu hao, Steven Gerrard baada ya mechi.
Makosa ya Gerrard yalisababisha bao la kwanza la Chelsea lililofungwa na Demba Ba na mashabiki wa The Blues wakawatia hasira Liverpool kwa kuimba jina la mchezaji huyo.

Mashabiki wa Chelsea wakizomea kwa jeuri ya ushindi wa 2-0

Mashabiki wakizipiga chanzo ni kuzomewa kwa Steven Gerrard

Polisi wakituliza ghasia

Baba akiongozana na kijana wake kutoka eneo la vurugu huku watu wakiendelea kuchapana nyuma yake

Polisi walilazimika kuwaachanisha watu wengine waliopelekana hadi chini katika mapambano yao

Polisi wakiwwka uzio baina ya mashabiki wa Liverpool na Chelsea

Mashabiki wa Liverpool wakisema na Polisi waliokuwa wakituliza ghasia hizo
No comments:
Post a Comment