Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, May 6, 2014

Wanne mbaroni kwa kukutwa na silaha za kivita Mara




Jeshi la Polisi mkoani Mara, limekamata bunduki saba zikiwemo za kivita pamoja na risasi 461 toka kwa watu wanne wakiwemo raia wawili wa nchi jirani ya Kenya, ambao wanatuhumiwa kuhusika katika mtandao mkubwa wa ujambazi wa kutumia silaha.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ferdinand Mtui, akizingumza na  jana Mei 5, 2014, alisema watuhumiwa hao walikuwa na bunduki moja aina ya SMG na risasi 23 silaha ambazo ni za kivita na nyingine za moto zikiwa zimekamatwa na wananchi kwa kushirikiana na Jeshi hilo katika oparesheni inayoendelea katika mkoa huo.
Hata hivyo, amesema watuhumiwa hao wakitokea katika Wilaya ya Tarime wakiwa na silaha hizo ambazo walikuwa wamezificha katika tenga lenye ndizi mbivu wakiwa tayari wamefika mjini Musoma kwa ajili ya kufanya uhalifu.
Amesema baada ya kukamatwa watu hao walianza kupigwa na wananchi kabla ya Polisi kutumia nguvu kwa kurusha risasi hewani na kuwatawanya wananchi hao, kwa ajili ya kuwakoa na kwamba wawili kati yao wamekufa wakati walipokuwa wanapelekwa hospitali kupatiwa matibabu kutokana na kipigo walichopata kutoka kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment