Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, June 2, 2014

ALIYEJIFANYA PROFESA WA CHUO KIKUU APANDISHWA KORTINI

Mkazi wa Tandika, Protace Mungodo (60) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Ilala, kujibu mashitaka ya kujifanya profesa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).
Wakili wa Serikali, Gloria Mwenda alidai mbele ya Hakimu John Msafiri kuwa Desemba 16 mwaka jana, maeneo ya Kariakoo Wilaya ya Ilala, Mungodo alijitambulisha kwa Patrick Mavika kuwa ni profesa wa chuo hicho. 


Mshitakiwa alikana mashitaka na alirudishwa rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana. Alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa, watakaosaini kulipa Sh milioni moja. Kesi itatajwa Juni 10 mwaka huu. 

Wakati huo huo, Mwajuma Hamis (40) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, kujibu mashitaka ya kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu. 

Karani Lucy Rutabanzibwa alidai mbele ya Hakimu Mwajuma Diwani kuwa Februari 2 mwaka huu maeneo ya Sokoni  Manzese, alijipatia Sh 90,000 na simu ya mkononi  ambayo haikubainishwa ni aina gani yenye thamani ya Sh 100,000 mali ya Asha Deogratius. 

Mshitakiwa alikana mashitaka na alirudishwa rumande baada ya kushindwa masharti ya dhamana, alitakiwa kuwa na wadhamini wawili, watakaosaini kulipa Sh 200,000. Kesi itatajwa Juni 12 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment