Kampuni ya Lifetime ya nchini Marekani imetangaza kipindi
kipya cha Televisheni kitakachoonyesha wazazi vijana wakijifungua porini bila
msaada wa madaktari wakati wa hatua zote za kujifungua lakini pia hawatakuwa na
malazi yoyote katika eneo hilo.
Kipindi hicho “Born in the Wild” kitatoa taswira kwa
wanawake na wanaume ambao wanaamini kuwa kujifunga mtoto katika mazingira
mazuri na kupatiwa huduma zote mbali na madaktari ni njia pekee.
Kipindi hicho kimetokana na video iliyopata umaarufu mkubwa
katika mtandao wa YouTube na kutazamwa mara milioni 20 ikionyesha mwanamke
akijifungua porini lakini tayari wakosoaji wa mambo wanasema kipindi hicho
kinaweza kutoa taswira ya kuhatarisha maisha ya wamama na watoto wanaopitia
mazingira hayo.
Picha hizi zimetolewa na gazeti la Daily mail UK.
No comments:
Post a Comment