Uwanja wa JAMHURI mkoani Morogoro utatumika kumuaga mtoto
Nasra Mvungi aliyefariki jana alfajiri
hospitali ya Muhimbili.
Hayo yamesemwa na Ofisa ustawi wa jamii mkoani Morogoro,
Oswin Ngungamtitu.
Amesema idara hiyo kwa kushirikiana na jeshi la Polisi imepanga kusimamia mazishi ya mtoto Nasra
Mvungi (4) maarufu katika magazeti kama mtoto wa boksi.
Mtoto huyo alifariki dunia leo katika hospitali ya Muhimbili
alikokuwa amelazwa kutokana na magonjwa mbalimbali yanayosadikiwa kusababishwa
kwake ndani ya boksi kwa zaidi ya miaka
mitatu.
Aidha kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro John Laswai
alisema kuwa baada ya kifo cha mtoto
huyo taratibu za kipolisi zitafanywa ikiwa ni pamoja na
kupata taarifa ya daktari ambayo itaeleza sababu za kifo cha mtoto huyo.
Alisema kuwa taarifa hiyo ikishatolewa itapelekwa kwa
wanasheria ambaye ataipitia na kuangalia sheria inavyosema na kama taarifa hiyo
itaeleza sababu za kifo kuwa imetokana na ukatili na watuhumiwa hao basi
watakamatwa na kesi itabadilika.
No comments:
Post a Comment