Tabasamu
kubwa: Mshambuliaji wa Man City ambaye hajatulia , Alvaro Negredo akicheka
wakati alipokuwa anapenda ndege kwenda Dundee.
KIKOSI cha
mabingwa wa England, Manchester City kimekwea pipa kwenda Dundee tayari kuanza
ziara yao ya maandalizi ya msimu huko Scottish.
Katika
msafara huo, pia umemjumuisha mshamabiliaji ambaye hajatulia kwa sasa, Alvaro
Negredo aliyeonekana kuwa katika morali nzuri.
Kikosi cha
Manuel Pellegrini kitacheza Dundee siku ya jumapili kabla ya kusafiri siku
inayofuata kwenda Edinburgh kucheza dhidi ya Hearts siku ya ijumaa.
Negredo
anayehusishwa kuondoka Etihad, alipigwa picha akipanda ndege binafsi ya Man
City, `City Jet` jana jioni, huku naye kipa mpya, Willy Caballero akiwemo
katika msafara huo.
Big bosi!: Kocha wa City, Manuel Pelligrin atakuwa na kikosi
chake nchini Scotland na baadaye atakwenda
America.
Kifaa kipya: Kipa mpya wa Man city, Willy Caballaro pia yumo
katika msafara wa klabu hiyo kwenda nchini Scotland kufanya maandalizi ya kabla
ya msimu.








No comments:
Post a Comment