Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, August 20, 2014

REAL MADRID YABANWA MBAVU KWA SARE YA 1-1 NA ATLETICO MADRID

 Rodriguez akishangilia bao lake na wachezaji wenzake wa Real Madrid
MFUNGAJI bora wa kombe la dunia lililomalizika majira haya ya kiangazi nchini Brazil, James Rodriguez alifunga bao lake la kwanza Real Madrid, lakini halikuweza kuipa ushindi timu hiyo ya Carlo Ancelotti dhidi ya Atletico Madrid katika mchezo wa kwanza wa Super Cup.Raul Garcia aliisawazishia Atletico kwa kuunganisha mpira wa kona zikiwa zimesalia dakika tatu tu mpira kumalizika.


Real wangeweza kushinda baada ya kufanya shambulizi hatari dakika za mwisho, lakini Mario Suarez aliweza kuzuia shuti lililopigwa na Dani Dani Carvajal.
Katika mchezo huo, mshambuliaji tegemeo wa klabu hiyo, Mreno, Cristiano Ronaldo alitolewa nje wakati wa mapumziko na kumpisha Rodriguez. Madrid.
 Ni mimi! Raul Garcia (kushoto) akishangalia baada ya kuisawazishia Atletico Madrid katika dimba la Bernabeu


James Rodriguez alijiunga na Real Madrid kutokea klabu ya Monaco majira haya ya kiangazi kwa dau la paundi milioni 60

No comments:

Post a Comment