Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, September 29, 2014

Mh. Lowassa amkaribisha Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania

 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimkaribisha wilayani Monduli Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada wakati alipowasili wilayani humo jana Jumapili Septemba 28,2014 kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na nchi hiyo.Balozi huyo aliahidi kusaidia vifaa vya kisasa katika hospitali mpya ya kisasa inayojengwa wilayani humo.
Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema (kushoto) akimkaribisha Balozi wa Japan nchini Tanzania,Mh. Masaki Okada hotelini hapo.Pembeni kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Monduli,Bw. Twalib Mbasha.


Balozi wa Japan nchini,Mh. Masaki Okada (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli,Twalib Mbasha (kulia) na Meneja wa Hoteli ya Emanyata mjini Monduli,Bi. Neema alikofikia balozi huyo na ujumbe wake katika ziara yake ya siku mbili wilayani humo.

No comments:

Post a Comment