Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, October 20, 2014

TAZAMA PICHA KIBAKA ALIYECHAPWA NA WANANCHI KWA KUIBA SIMU

Kijana Mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Omar mkazi wa Mafisa Morogoro,ambaye ni dereva wa boda boda mwishoni mwa wiki iliyopita alipokea  kichapo  kutoka kwa wananchi wenye hasir akidaiwa kumpora simu mwanamke mmoja nayedaiwa kuwa mwanafunzi wa chuo Kikuu Cha Kilima Cha Sokoine’ SUA’ 
Tukio hilo limetokea ijumaa iliyopita  Eneo  Mazimbu  FK  ambapo Mwanafunzi  huyo alikuwa akitembea kuelekea chuoni huku akiongea na simu hivyo Omar aliyekuwa amempakia mwenzake kwenye pikipiki walimpora simu kwa kutumia pikipiki hiyo.
















Na Dustan Shekidele,Morogoro.
 Wakihojiwa na Mwandishi wetu eneo la tukio mashuhuda wa tukio hilo wasliema”huyu dada alikuwa akieleka SUA huku akiongea na simu ghafla boda boda huyu aliyekuwa amembeba mwenzake nyuma walimpitia  kumpora simu dada huyu na kukimbia nayo ambapo dada alipiga kelele za mwizi na boda boda wa kijiwe la FK waliwasha pikipiki zao na kuwafukuza ambapo walifanikiwa kuwakamata eneo hili la mazimbu reli ya pili ambapo mwenzake aliyempakia nyuma alifanikiwa kuruka katika pikipiki na kukimbia na kumuachia msara mwenzake.  
Katika hatua nyingine mmoja wa boda boda aliyefanikisha kukamtwa kwa kibaka huyo alisema' Hii ni kazi ya boda boda ni kazi  kama kazi nyingine na tunashukuru serikali inatutambua lakini kuna baadhi ya bodaboda wanatupaka matoke kw akufanya mambo ya wizi huku wakitumia mgongo wa boda boda ndio maana tulivyoshuhudi tukio hili tumeamu kuteketeza mafuta yetu na kuwafukuza vibaka hawa na kufanikiwa kuwakamata"alisema  Bw Juma ldd

Mwandishi wa mtandao huu alipiga simu polisi kwa lengo la kumuogoa mwizi huyu ambapo fasta Defenda lilifika na kumchukua kibaka huyu ambapo baadhi ya watu wanaomfahamu walidai anaegesha pikipiki wake kijiwe cha Tumbaku lringa Road  na kwamba pikipiki hiyo alikabidhiwa kwa mkataba wa kwama mmoja ambapo mwaka ukimaliki pikipiki ni mara yake na kwamba alibakiza miezi miwili kukamilisha mkataba huo.

 Afisa mmoja wa jeshi la polisi aliyeom,ba hifadhi ya jina lake alimtonya mwandishi wetu kwamba boda boda huyo alikata roho siku iliyofuata

No comments:

Post a Comment