Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 8, 2015

VALDES KUSAINI MAN UTD

Kipa wa zamani wa Barcelona Victor Valdes amekubali kujiunga na Manchester United. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Spain, ambaye amekuwa akifanya mazoezi na Manchester United katika jitihada za kupona jeraha la goti, amekubali mkataba wa miezi 18. Valdes, 32, alishinda makombe sita ya La Liga, na matatu ya Champions League akiwa na Barcelona, kabla ya mwisho wa msimu uliopita ambapo mkataba wake ulimalizika. Mkataba huu huenda ukasababisha kipa wa akiba wa United 


Anders Lindegaard kuondoka Old Trafford. Hatua hiyo pia inaleta maswali mengi kuhusu hatma ya David De Gea, 24, ambaye alikuwa mchezaji bora wa timu hiyo msimu uliopita na amekuwa aking'ara msimu huu pia.

Mkataba wake utaisha mwaka 2016, ingawa taarifa kutoka United zinasema hawana wasiwasi na kipa huyo kuongeza mkataba wake.

No comments:

Post a Comment