Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, August 25, 2015

KUNANI TENA KATI YA DIAMOND NA MTANGAZAJI DIVA?

Msanii wa Kizazi kipya Diamond Platnumz na Mtangazaji wa Clouds Fm, Diva Loveness love wamejikuta wakirushiana maneno hewani kwasababu ya ugomvi wao chinichini ambao unaonekana ni wa muda mrefu.
Vita hiyo ya maneno ya watu hao ambao waliwahi kuimba wimbo wa pamoja ‘Piga simu’ imeanza baada ya Mtangazaji wa kipindi cha XXL, Bdozen kuwauliza kama washamaliza tofauti zao (hazijulikani) ndio Diamond akadakia na kumuuliza mtangazaji huyo kwanini huwa anamsema vibaya baada ya hapo ndio wakaanza kurushiana maneno makali.

 
Diamond alisikika akisema anawaza kwanini hakumk*za labda ndio heshima ingekuwepo lakini Diva alijibu hilo haliwezekani kwasababu Diamond sio Type yake. Mtangazaji wa kipindi cha XXL Bdozen alilazimika kuzima Mike kwasababu hakukuwa na dalili za watu hao kupatana licha ya kujaribu kuwapatanisha hewani.
Hatujui kilichoendelea lakini baada ya Muda kidogo, Diva aliamia kwenye mtandao wa Twitter, akialalamika kuwa Diamond alimtishia kumpiga
Diamond hajamjibu hadi now lakini manager wa Diamond, Salaam amemjibu Diva kuwa Twitter si mahala sahihi ya kupeleka malalamiko yake, na hizi ndio Tweets zake

No comments:

Post a Comment