Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, September 1, 2015

HATIMAYE AGUSTINO RAMADHAN ATOA YA MOYONI KUHUSU KUHAMA CCM


Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu, Jaji Agustino Ramadhani, amesema hajawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM).Aliyasema kuhusu taarifa zilizoenea kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, kwamba yeye na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, wapo katika mipango ya kuhamia kambi ya upinzani.
Jaji Ramadhani ambaye alikuwa mmoja kati ya makada 42 waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM, jina lake lilikatwa na Kamati ya Maadili kabla ya kufikishwa mbele ya Kamati Kuu (CC) ya chama hicho.
Jaji Ramadhani ambaye alikuwa kimya tangu mchakato huo


 
 umalizike, alisema taarifa hizo na yeye ameziona kwenye mitandao.
Hizo taarifa hata mimi niliziona kwenye mitandao ya kijamii, kwamba mimi na Mh. Bilal tutazungumza na vyombo vya habari kutangaza kuhama chama na kwamba tutasindikizwa na mzee Warioba (Jaji Joseph Warioba), wanaoeneza hayo ni watu wasiyo na adabu, sijawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama CCM, alisema.
Alisema yanayoenezwa kwenye mitandao dhidi yake, kuhusiana na kuhama chama hayana ukweli wowote. CHANZO UDAKU ESPECIALLY

No comments:

Post a Comment