Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, October 19, 2015

Mwalimu ampiga mwandishi



Mwalimu Willibroad Samson wa Shule ya Sekondari Kitunda iliyopo Wilaya ya Ilala, akimdhibiti mwanafunzi, Elia Simion aliyekuwa akipigana na mwenzake. Picha na Tumaini Msowoya 

Dar es Salaam. Mwandishi wa Mwananchi, Tumaini Msowoya jana alipigwa ngumi kadhaa kichwani na mwalimu wa Shule ya Sekondari Kitunda wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi.
Msowoya alipigwa na mwalimu aliyefahamika kwa jina la Willibroad Samson alipokwenda shuleni hapo kufuatilia madai kwamba baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo, wiki iliyopita waliandikishwa na kupewa vitambulisho vya kupigia kura katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Msowoya alisema kwamba tukio hilo lilitokea kati ya saa 4.30 na saa 5.00 asubuhi karibu na jengo la ofisi za walimu. “Nilifika shuleni pale saa 3.00 asubuhi kwa ajili ya kuonana na mkuu wa shule, sikumkuta ila nilipokewa na makamu mkuu wa shule. Lakini wakati nikiendelea na mazungumzo ofisini kwa mwalimu huyo tulisikia wanafunzi wakipiga kelele,” anasema Msowoya.
Alisema kuwa alipotaka kutoka nje baada ya kukamilisha mazungumzo na makamu mkuu wa shule alisikia kelele zikipigwa huku mawe yakirushwa na kupiga jengo la ofisi ya walimu wa shule hiyo. “Hivyo tukaufunga mlango na baada ya muda mfupi nilitoka nje na kushuhudia wanafunzi wawili wakipigana huku wenzao wakishangilia,” alisema.
Kwa mujibu wa Msowoya, alianza kupiga picha za tukio hilo, na punde alimwona mwalimu Samson akiamulia wanafunzi waliokuwa wanagombana. Pia, alimwona mwalimu huyo akimdhibiti Elia Simion, mmoja wa wanafunzi wa kidato cha kwanza waliokuwa wanapigana huku akitoka damu mdomoni baada ya kupigwa na mwenzake.

Katika tafrani hiyo, Msowoya alisema mwalimu huyo alimpiga huku akimvutia katika ofisi ya walimu, lakini walimu wengine waliingilia kati kumzuia.
Kutokana na kipigo hicho, alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Kitunda ambako alipewa fomu ya PF3, kisha akapatibiwa katika Zahanati ya Kitunda.
Alipoulizwa makamu mkuu wa shule aliyejitambulisha kwa jina moja la Masatu kuhusiana na tukio hilo alikiri kushuhudia lakini akasema mwalimu aliyefanya tukio hilo anajitolea kufundisha, siyo mwajiriwa wao.
Mwalimu Samson alipoulizwa sababu za kumpiga mwandishi alisema kuwa alikasirishwa na kitendo cha kupigwa picha wakati akiamulia ugomvi wa wanafunzi. Hata hivyo, kuhusu madai kwamba wanafunzi waliandikishwa na kupewa vitambulisho kwa ajili ya kupiga kura, Masatu alikanusha akidai wanafunzi walipigwa na kupewa vitambulisho vya shule ambavyo mpigaji ni mtu binafsi.chanzo Mwanainchi

No comments:

Post a Comment