Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 11, 2015

JIJI LA MBEYA LAJIPANGA KUKUSANYA KODI KATIKA MRADI WA SOKO JIPYA LA MWANJELWA

Kaimu Mkurugenzi jiji la Mbeya Dkt,Samuel Razalo
Na EmanuelMadafa,Mbeya
HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya, imesema imejipanga vyema katika  kuhakikisha  mradi mkubwa wa soko jipya la mwanjelwa unasimamiwa kikamilifu kwa kufuata  taratibu za serikali sanjali na mikataba  iliyoingia na benki ya CRDB  kwa kipindi cha miaka 15.

Mradi  huo wa soko la kimataifa la Mwanjelwa lililopo jijini Mbeya  ujenzi wake imefikia  asilimia 99 hivyo upo katika hatua za mwisho za kukamilika kwake.

Akizungumza  ofisini kwake  , Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Dkt. Samweli Razalo, amesema licha ya soko hilo kukamilika lakini mchakato wake wa uendeshaji utazingatia taratibu za halmashauri na mkataba walioingia na benki ya CRDB.


Amesema  hatua  hiyo, inatokana na halmashauri ya Jiji hilo kukopa kiasi cha shilingi Bilioni 13 kutoka benki ya CRDB na kufanikisha ujenzi wa soko hilo ambao umedumu kwa  zaidi ya miaka 10 tangu lilipoteketea kwa moto.


Amesema, benki hiyo kwa kukubaliana na halmashauri imepanga kiasi cha kodi kitakachopaswa kulipwa na wafanyabiashara  kuanzia shilingi elfu moja kwa siku hadi shilingi 500,000 kwa mwezi.

Amesema Wafanyabiashara ambao watatumia meza watatakiwa kulipa ushuru wa shilingi 1000 kwa siku huku wale wa maduka watalipa kiasi cha shilingi 500,000 kwa mwezi na wauza nyama watapaswa kulipa kiasi cha shilingi 400,000 kwa mwezi,”alisema.

Amesema , awali halmashauri hiyo ilipokea maombi kutoka kwa wafanyabiashara ambao walikuwa wakiomba kupunguzwa kwa gharama za tozo hizo kwani ziko juu ukilinganisha na hali ya uhumi wa sasa.

Amesema, halmashauri iliyachukua maombi hayo na kuyawasilisha kwenye mamlaka husika ya benki ya CRDB hivyo wanasubili majibu na kuwataka wafanyabiasha kuwa wapole wakati wanasubili majibu hayo kutoka kwenye uongozi wa benki hiyo.

Soko la Mwanjelwa liliteketea kwa moto mwaka 2006 na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha kutoka kwa wafanyabiashara zaidi ya 2000 walionguliwa maduka yao na ujenzi wake kuanza mwaka 2008..

Mwisho.

Muonekano wa Mradi wa Soko la Mwanjelwa Jijini Mbeya ambapo ujenzi wake bado unaendelea.(JAMIIMOJABLOG MBEYA)

No comments:

Post a Comment