Sumaye akionyesha Kadi ya Chadema mara baada ya kukabidhiwa
WAZIRI
Mkuu mstaafu wa awamu ya Tatu, Frederick Sumaye ametangaza rasmi
kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kukabidhiwa na
kadi ya uanachama wa chama hicho.
Sumaye,
ambaye alijiunga na vyama vya Upinzani vinavyounda Ukawa miezi mine
iliyopita wakati wa Kampeni za uchaguzi mkuu uliomalizika Octoba 25
mwaka huu,ambapo wakati huo Sumaye alikihama chama cha Mapinduzi CCM
huku akishindwa kuweka wazi chama kipi alikiunga nacho.
Sumaye
ametangaza hatua hiyo leo mkoani Arusha wakati wa kuhitimisha Kampeni
za uchaguzi mdogo wa Ubunge jimbo la Arusha mjini,ambapo amesema
amejiridhisha pasipo shaka kuwa Chadema ndiyo chama pekee chenye kuweza
kumletea maendeleo Mtanzania jambo lilofanya akihamie chama hicho huku
akimpongeza Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kuwa ndiye
anayeweza kukijenga chama bila kutetereka.
Chanzo:Fullhabari
Chanzo:Fullhabari
No comments:
Post a Comment