Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, December 21, 2015

TAZAMA PICHA 10:::WAZIRI UMMY MWALIMU AVAMIA HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO MKOANI TANGA, KUKAGUA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA

IMG-20151220-WA0011
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wahudumu wa afya (jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi) wa dirisha la dawa katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga alipofanya ziara ya kushtukiza mchana wa  Disemba 20, 2015.
-Atoa wiki mbili wawe wamefunga mashine ya kukusanya mapato kwa njia ya Kielektroniki ili kudhitibiti upotevu wa mapato yanayotokana na wananchi kuchangia huduma za afya.
IMG-20151220-WA0012
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na mmoja wa wakina mama anayemhudumia mwanae katika wodi ya watoto Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga alipofanya ziara ya kushtukiza  Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0019
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akimsikiliza mmoja wa akina mama aliyelazwa kwenye wodi ya wazazi wakati wa ziara ya kushtikiza aliyoifanya mchana wa Desemba 20, 2015 katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga.
 
IMG-20151220-WA0020
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO), Dkt. Clement Marceli akimwelezea changamoto wanazokabiliana nazo katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani Tanga Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (hayupo pichani).
IMG-20151220-WA0017
Daktari aliyekuwa kwenye mafunzo, Dkt. Zuberi (Medical Intern) akitoa maelezo ya namna wanavyohudumia wananchi wanaofika hospitalini hapo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu (kulia) aliyefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mchana  Desemba 20, 2015 ambapo Waziri huyo alikutana na changamoto utoro wa madktari wa zamu kutokuwepo kwenye kituo chao cha kazi katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga.
IMG-20151220-WA0016
IMG-20151220-WA0019
Mratibu wa Hospitali ya Rufaa ya Bombo, mkoani Tanga kutoka Idara ya Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Ibrahimu Maduhu (mwenye tai) akitoa maelezo kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu namna wanavyokabiliana na changamoto ya kuzuia vifo vya mama na mtoto katika hospitali hiyo wakati wa ziara ya kushtukiza iliyofanywa na Mh. Ummy Mwalimu katika wodi ya wazazi  Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0014
Baadhi ya madaktari waliokuwa mafunzoni wakizungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu aliyefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo, mkoani Tanga  Disemba 20, 2015.
IMG-20151220-WA0023
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu akipitia orodha ya mahudhurio ya zamu za Madaktari na Wauguzi ambao wengi hawakuwepo kazini wakati wa ziara yake ya kushtukiza katika Hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga aliyoifanya  Disemba 20, 2015.

No comments:

Post a Comment