Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, January 29, 2016

Moto wateketeza bweni la Shule ya Sekondari Edward Lowassa

Bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari ya Edwaed Lowassa iliyoko wilayani Monduli mkoani Arusha limeteketea kwa moto na wanafunzi zaidi ya 70 wa kidato cha kwanza wamelazimika kupewa likizo ya wiki moja baada ya kukumbwa na hofu iliyotokana na moto huo.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw Salum Selemani amesema moto huo ambao umetekeza mali zote za wanafunzi na majengo unaodaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme za ulianza saa nne usiku wakati wanafunzi wakiwa darsani na hakuna aliyejeruhiwa japo baadhi yao walikumbwa na hofu iliyosababisha wapoteze fahamu na kukimbizwa hosipitali.


Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Monduli ambaye pia ni mkuu wa wilaya Bw Fransis Miti amesema kwa sasa wanafunzi wote wako salama na wamefikisa hatua ya kuwapa likizo fupi ili waweze kutulia wakati jitihada kuwawezesha kuendelea na masomo zikifanyika.

Chanzo: ITV

No comments:

Post a Comment