Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, February 1, 2016

PICHA 3:::Meli kubwa iliyoinama yazua wasiwasi Ufaransa

Meli hiyo ina tani 300 za mafuta
 Meli ya kubwa iliyoegemea upande mmoja inakaribia kufika katika pwani ya Ufaransa, maafisa wa bahari wanasema, ingawa kuna matumaini ya kuiokoa kabla ya kuzama.
 Meli hiyo kwa jina Modern Express ambayo, imesajiliwa Panama, ilianza kulala upande mmoja Jumanne baada ya kutokea kwa hitilafu za kimitambo.
 Mabaharia wote 22 wameondolewa kutoka kwenye meli hiyo.


Meli hiyo imo katikati ya Bordeaux na Biarritz katika bahari ya Atlantic
 Juhudi za kuisimamisha zimefeli, lakini maafisa wanasema jaribio jingine litafanywa leo Jumatatu.
 Juhudi za leo zikishindikana, basi meli hiyo itagonga pwani ya Ufaransa kati ya Jumatatu usiku na Jumanne asubuhi. 
 
 Hali mbaya ya hewa ilitatiza juhudi za uokoaji Jumapili.
 Meli hiyo imebeba tani 3,600 za mbao na mashine kadha za uchimbaji, na imeinama kwa pembe ya kati ya nyuzi 40 na 50.
 Ina tani 33 za mafuta.


Mabaharia wote wameondolewa melini
Mwaka 2002, meli ya kusafirisha mafuta kwa jina Prestige ilizama karibu na pwani ya Uhispania na kumwaga mafuta tani 50,000 na kuchafua eneo kubwa la bahari.Chanzo BBC

No comments:

Post a Comment