Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Tuesday, February 16, 2016

UN CLUBS TANZANIA NA PROF. NDALICHAKO WATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA KURASINI

Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (kulia) akimkabidhi msaada kwa mlezi wa kituo cha kulelea watoto Bi. Jack Omary(kushoto) ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii kituo cha taifa cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Kurasini, hafla hii imefanyika katika siku ya wapendanao. Misaada hyo imetolewa na vijana wa UN Clubs Tanzania Network kwa kanda ya Dar es salaam pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.(Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog).

UN Clubs Tanzania Network kanda ya Dar es Salaam wakishirikiana na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako wametoa msaada kwa kwenye kituo cha kulelea watoto yatima cha Kurasini kwenye siku ya wapendanao ili kuonesha upendo mkubwa kwa watoto hao. Vijana hao wa UN Club Tanzania Network wanafanya kazi siku ya wapendanao nchi nzima za kusaidia jamii na vijana wa jijini Dar es salaam wameungana na watoto wa kituo cha Kurasini kwa kutoa msaada na wanafunzi hao wametoka katika shule za sekondari za Zanaki, Azania, Benjamin na Jangwani. Akizungumzia msaada huo, Afisa Ustawi wa Jamii katika kituo hicho. Jack Omary aliwashukuru kwa 

 
kuwatembelea siku ya wapendanao maana kuna watu wengine wanaitumia siku ya wapendanao kwenye starehe na hata kutumia pesa bila kuangalia kuna watu wanahitaji msaada. Nae Stella kutoka UN Clubs Tanzania amesema lengo la kuja katika kituo cha watoto yatima cha Kurasini nikujumuika na hao watoto ambao hawana wazazi na pia watoto wenye shida mbalimbali.
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo (kushoto) akiwakabidhi misaada watoto wa Kituo cha Kurasini, katikati ni mtoto Aboubakary Seif ambaye alipokea kwa niaba ya watoto wenzake.

Alisema inabidi kuwakumbuka hasa kwenye siku kama za wapendanao kwani kuna watu wanatumia pesa nyingi kwenye starehe kuliko kutoa misaada kwa watoto wenye mahitaji maalumu hasa wazee,walemavu na hata watoto yatima. Mtoto Aboubakary Seif anayelelewa katika kituo hicho cha Kurasini amewashukuru UN Clubs Tanzania Network Pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako kwa kuwaona kama watu katika jamii wanakubalika hasa kwenye siku ya wapendanao.
Mwenyekiti wa Jangwani Fema, Jeniffer Kayombo (kushoto) pamoja na Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo wakiwakabidhi zawadi watoto wa kituo cha Kurasini jana ikiwa ni siku ya wapendanao.
Amesema wao wamesijsikia furaha kutembelewa na vijana wenzao na kuwapa moyo hasa kwa kusoma kwa bidii ili kufikia malengo waliyojiwekea. Pia aliwaomba watu wengine wenye uwezo waje kutoa msaada maana matatizo ni mengi na matatizo hayo yatatatuliwa kwa misaada ya wadau mbalimbali.
Zuwena (kushoto) akimkabidhi mpira mtoto aliyewawakilisha wenzake kituoni hapo.
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akizungumza jambo mbele ya watoto (hawapo pichani) walipowatembelea watoto hao wenye mahitaji maalumu kwenye kituo cha Kurasini, jijini Dar es Salaam katika siku ya wapendanao.
Mwenyekiti wa Jangwani Fema, Jeniffer Kayombo akiwaasa watoto kusoma kwa bidii ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea.
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akiwagawia watoto hao soda pamoja na biskuti ambapo Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako pamoja na vijana wa UN Clubs Tanzania Network kwa kanda ya Dar es salaam walitoa zawadi hizo.
Baadhi ya vijana wa UN Clubs Tanzania Network kwa kanda ya Dar es salaam kutoka katika shule za Sekondari za Jangwani, Zanaki, Benjamini na Azania wakiwagawia zawadi watoto wenye mahitaji maalumu.
Hakika ilikuwa ni siku ya furaha sana kwa watoto yatima wanaolelewa kwenye kituo cha Kurasini.
Hii ndio misaada iliyotolewa katika kituo cha kululea watoto yatima cha Kurasini jijini Dar es Salaam.
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akiwa kwenye picha ya pamoja na Umoja wa vijana wa youth advisory board (FEMA YAB) walipotembelea watoto yatima katika kituo cha Kurasini Jijini Dar es Salaam.
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo akiwa kweye picha ya pamoja na watoto wa kituoni hapo.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment