Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, February 24, 2016

WATU WANAOSADIKIKA KUWA MAJAMBAZI WAPORA MILIONI 12 JIJINI DAR

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro.(Picha na Maktaba)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
MKAZI wa Mafinga,  David Isack ( 32) alivamiwa na majambazi na kuporwa sh.milioni 12 ambazo alikuwa akipeleka katika Benki ya  DTB, ambapo alivamiwa na  watu  watano wanatuhumiwa kuwa ni majambazi wakiwa na usafiri wa pikipiki  mbili aina ya boxer.

Akizungumza na waandishi wa habari ijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro amesema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 12 mwaka huu katika eneo la Uwanja Ndege , katika kurupushani za kutaka kuchukua fedha hizo walitokea askari na kuwazingira na kisha kuanza kukimbia na kuweza kudondosha bunduki aina ya SMG pamoja na risasi 24 ambazo zilitakiwa kutumika katika tukio hilo.


Amesema askari walipowakamata wananchi walikusanyika katika tukio hilo na kuanza kuwapiga watu wanaodaiwa kuwa majambazi mpaka kupoteza maisha kutokana kushambuliwa huko na wengine watatu waliweza kukimbia na kiasi hicho cha fedha.

Kamishna Sirro amesema Isac alikuwa akitokea benki ya NMB na kwenda kupeleka fedha hizo katika benki ya DTB iliyopo Quality Plaza.

Katika operesheni nyingine imefanikiwa kukamata bastola moja ambayo ilipatikana  Februari 19 mwaka huu maeneo ya Kiwalani Kwa Gude kutokana na polisi kupata taarifa juu ya watu kujificha katika kichaka kwa ajili ya kufanya uhalifu  na baada ya kugundua polisi wapo eneo hilo walikimbia na kuacha silaha hiyo na jeshi la polisi linafanyia kazi mmiliki wa silaha.

Hata hivyo Jedhi la Polisi Kanda Maalumu linawashikilia watu wane wanaodaiwa kuwa ni majambazi sugu waliowakamata eneo la  Buguruni kwa Mnyamani ambao ni Mohamed Hassan maarufu kwa jina Kidali (21)Mkazi wa Vingunguti Speco,Hamis Alli (20) Mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani, Adam Salum (23) Mkazi wa Buguruni  kwa Madenge, Bakari Hamis (19) Mkazi wa Buguruni.

Aidha amesema katika taarifa usalama Barabarani wameweza kukusanya zaidi ya Sh. Bilioni moja ya ni fedha iliyotokana na makosa ya magari kuanzia Januari 02 hadi Februari 22 mwaka huu.

CHANZO: MICHUZI BLOG

No comments:

Post a Comment