Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, March 9, 2016

JE WAJUA TIMU YA TOTO AFRICANS YA JIJINI MWANZA NDIYO TIMU MASKINI KULIKO ZOTE LIGI KUU NCHINI?

Kocha wa Timu ya Soka ya Toto Africas ya Jijini Mwanza inayoshiriki Liku Kuu nchini, John Tegete (Wa pili kulia) akiwa na "Wananzengo" kutoka Jijini Mwanza ambao wanatarajiwa kuwa wadau wapya wa timu hiyo.
Na:George Binagi-GB Pazzo
Kwa Mjibu wa Tegete, Toto Africans ndiyo timu Maskini kuliko zote zinazocheza Liku Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Bajeti yake kwa Mwaka ni zaidi ya Shilingi Milioni 495 lakini mapato yake kwa mwaka ni takribani shilingi Milioni 180. 

Inakadiriwa kuwa hakuna timu nyingine yenye matapo ya chini kama hayo miongoni mwanza timu za Liku Kuu Tanzania Bara hivyo kwa hali hiyo Toto Africans inapitia wakati mgumu katika kujiendesha kuliko inavyofikiriwa.


Pamoja na ugumu huyo, Toto Africans iko nafasi ya Tisa kati ya Timu 16 zinazoshiriki Ligu hivyo hivyo kwa mazingira inayopitia inastahili kuitwa timu bora ambayo haipaswi kutelekezwa na wadau wa soka Jijini Mwanza wakiwemo Wananzengo ambao wameonyesha nia ya kushirikiana na timu hiyo.

No comments:

Post a Comment