Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, June 28, 2012

Mwinyi ajitoa machozi band


Aliyekuwa mwimbaji wa bendi ya Machozi inayomilikiwa na mwanadada Lady Jaydee amesema sababu za kujiondoa kwenye bendi hiyo ni kutokana na ubabaishaji mkubwa unaoendelea.
Akiongea na Clouds Fm jana, Mwinyi amesema hakufukuzwa kwenye bendi hiyo bali aliamua kuondoka mwenyewe baada ya kuchoshwa na ahadi za uongo kutoka kwa uongozi wa bendi hiyo.
Amesema kuwa kwa muda mrefu ameuvumilia ule aliouita ‘mkataba wa kijinga’ aliokuwa anautumikia kwa malipo ya kila mwisho wa wiki ambayo hata hivyo yalikuwa kiduchu na wakati mwingine alikuwa hakuti bahasha yake.
Mwinyi ambaye pia ni model, alieleza kuwa pamoja na bendi nyingi kutangaza nia ya kumchukua kwa ahadi za mkwanja mrefu, aliendelelea kuuvumilia ‘uswahili’ wa Machozi bendi na heshima yake kwa Lady Jaydee huku akiimba ‘for fun tu’.

Amesema Lady Jaydee alikuwa akimwonesha dharau kubwa na kujiona yuko juu wakati bendi yakeisingefika hapo ilipo bila ya mchango wake.
Mwimbaji huyo aliongeza kwa kusema kuwa sifa za nje za bendi hiyo ni kubwa lakini ukweli wa ndani ni kuwa haina lolote zaidi ya uswahili na ubabaishaji mwingi.
Mwinyi si msanii pekee aliyejitoa hivi karibuni kwenye bendi hiyo ya Machozi.
Mwimbaji mwingine aitwaye Sam ameamua kwenda kutafuta riziki kwenye bendi ya Skylight inayomilikiwa na mshiriki wa zamani wa Tusker Project Fame,Aneth Kushaba kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi milioni sita.
Clouds Fm walipojaribu kumpigia simu Gadner Habash kuelezea masuala hayo aliwapa jibu la ‘NO COMMENT’.

No comments:

Post a Comment