Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Friday, December 14, 2012

Rais Kikwete akabidhi nyumba mpya 35 za walioathirika na milipuko ya mabomu ya Gongo la Mboto.



 

Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto.
Bila kujali mvua kubwa inayonyesha, Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa  kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mmoja wa walionufaika na hatua ya serikali ya kujenga  nyumba mpya 35 kwa ajili ya  waathirika wa mabomu Gongo la Mboto  katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala leo Desemba 13, 2012. Mama huyu ambaye alipoteza mume, amejengewa nyumba ya vyumba vitano pamoja na fremu ya duka.
Pichani juu na chini ni Baadhi ya  nyumba mpya 35 ambazo serikali imewajengea waathirika wa mabomu Gongo la Mboto katika eneo la Msogole, Toangoma, Wilaya ya Ilala kama zinavyoonekana  leo Desemba 13, 2012 baada ya kuzinduliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.(PICHA NA IKULU).

No comments:

Post a Comment