Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, February 13, 2013

YANGA YAISHUSHIA KIPONDO AFRICAN LYON YAICHAPA MABAO 4-0



 Mshambuliaji wa Yanga, Hamis Kiiza (kulia) akichuana kuwania mpira na beki wa African Lyon, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 4-0, mabao 2, yakifungwa na Jerry Tegete, bao la 3 limefungwa na Didier Kavumbagu na bao la 4, limefungwa na Nizar Khalfan.
 Pande la maudhi, Haruna Niyonzima (katikati) akitoa pasi ya maudhi huku huku akiwa katikati ya wachezaji wa African Lyon.
 Kipa wa Yanga, Ally Mustapher, akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
 Yanga, wakikosa bao la wazi.
 Nizar Khalfan, akikimbia kushangilia bao lake, huku akipongezwa na Haruna Niyonzima.
 Jerry Tegete (katikati) akipongezwa na wenzake, baada ya kufunga bao la 2.
 Sehemu ya mashabiki wa Yanga.
 Kocha wa African Lyon, Salum Bausi, akiwa katikati ya uwanja akiwatuliza wachezaji wake kukubali kupigwa penati, waliyokuwa wakiigomea, huku wakimzonga refa.
Wachezaji wa African Lyon, wakimzonga mwamuzi, baada ya kutoa maamuzi ya kupigwa penati.

No comments:

Post a Comment