Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, March 24, 2013

MAANDAMANO YA CHADEMA KESHO: MBOWE ADAI YAKO PALE PALE NA WATAANDAMANA MBELE YA RAIS WA CHINA




LICHA ya serikali kuyapiga marufuku maandamano yaliyoratibiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuishinikiza kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Naibu wake wajiuzulu kutokana na matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne 2012, chama hicho kimesema yapo pale pale.

Chama hicho kimewaomba wananchi wote waliochoshwa na kufelishwa kwa watoto wao, kunyimwa elimu bora wajitokeze kuandamana kwa nguvu zote, na wanafunzi wote waliofeli pia wajitokeze kudai elimu bora kwani ni haki yao. 

Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana na kutoa msimamo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alisema “wananchi wajitokeze kwa wingi ili kilio chao kisikike duniani kote.” 

Alisisitiza kuwa maandamano hayo yatafanyika mbele ya ugeni wa Rais wa China, Xi Jinping ili kufikisha kilio hicho na kamwe haikubaliani na sababu ya serikali kuyazuia kwa sababu ya ugeni huo. 

No comments:

Post a Comment