Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, March 23, 2013

SAKATA LA KIBANDA: MAGAZETI YA MTANZANIA NA TANZANIA DAIMA HATARINI KUFUNGIWA


 



HATUA ya vyombo vya habari kulivalia njuga suala la kutekwa, kuteswa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda haiwafurahishi watendaji wa serikali.

Vyombo kadhaa vya habari yakiwemo magazeti, vimekuwa na habari, makala na maoni mfululizo kuisukuma serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi iwasake na kuwafikisha mahakamani wahusika wa tukio la Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006).
Katika habari hizo, vyombo hivyo vinaeleza kushangazwa na kitendo cha Jeshi la Polisi kushughulikia matukio mepesi haraka na kwa kutumia nguvu nyingi, huku sakata la Kibanda na lile la Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka uchunguzi wake ukidorora.
Msukumo huo wa vyombo vya habari kuvisakama vyombo vya dola na baadhi ya vigogo serikali kuhusika na matukio hayo umepokelewa kwa mtazamo hasi.
Habari za uhakika zinasema kuwa vigogo kadhaa wameanza kuhaha kupanga mikakati ya kuvizima vyombo hivyo, hususani magazeti ya Tanzania Daima na Mtanzania ambayo yamekuwa mstari wa mbele kuandika sakata hilo.

No comments:

Post a Comment