Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Saturday, March 23, 2013

RAIS WA CHINA KUSAINI JUMLA YA MIKATABA 17 NCHINI




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Na Eeuteri Mangi na Hussein Makame - Maelezo
Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping anataraija kuanza ziara ya kihistoria nchini tangu kuapishwa kwake kuitumikia nchi hiyo ambapo katika ziara hiyo atasaini mikataba 17 ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya Serikali za Tanzania na nchi hiyo.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe alisema kuwa ziara hiyo ni ya kwanza barani Afrika kwa Rais huyo mpya wa China baada ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo Machi 14 mwaka huu.

Lengo la ziara hiyo ambayo itaanza tarehe 24 hadi 25 Machi mwaka huu ni kukuza uwekezaji na biashara baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

Baadhi ya Mikataba hiyo itahusiana na uboreshaji wa sekta ya viwanda, kilimo hasa cha tumbaku ikiwemo kuwatafutia soko wakulima kutoka mikoa ya Tabora na Ruvuma ili waweze kuuza zao hilo katika soko la China.

No comments:

Post a Comment