Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, May 13, 2013

SAFARI YA WANAJESHI WETU HUKO KONGO


Watanzania  tunafuraha kubwa  kwa  sababu wapiganaji wa Jeshi letu  la Wananchi Tanzania (JWTZ) wamewasili mji wa Goma, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kujiunga na mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani  wakiwa  salama....

Wiki iliyopita, Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete alikabidhi Bendera kwa Kiongozi wa Bataliani ya wapiganaji wa JWTZ wanaokwenda nchini humo, kwenye hafla iliyofanyika Msangani Kibaha, Mkoa wa Pwani.....
Siku moja kabla ya kufika kwa kikosi cha pili cha Tanzania (cha kwanza kilienda kimya kimya) waasi wa M23 waliendesha kampeni kubwa sana ya kuhamasisha wananchi wa GOMA waandamane kupinga ujio wa askari wa Tanzania mjini GOMA...
Kiongozi wa siasa wa M23 akiongea na wakazi wa Kibumba na huku hutuba yake ikirushwa na redio inayomilikiwa na waasi na kusikika mjini GOMA ,aliwaasa wakazi wa GOMA wafanye maandamano makubwa siku vikosi vya TANZANIA vitakapowasili...
CHAKUCHEKESHA  ni kwamba, tofauti na waaasi walivyo tegemea , hakuna Mtu hata mmoja aliye andamana! Hii inaonyesha wazi  kuwa waasi hawa wameshapoteza ushawishi walio kuwa nao hapo awali....

No comments:

Post a Comment