Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, July 22, 2013

MLIPUKO WA BOMU KATIKA UWANJA WA NDEGE BEIJING


Shirika la habari nchini China limesema mtu mmoja ameripua bomu la kutengezwa nyumbani leo katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Beijing katika lango nambari tatu lakini mbali na mshukiwa huyo,hakuna mtu mwengine aliyejeruhiwa katika kisa hicho.
Shrika hilo la Xinhua limewanukuu walioshuhudia wakisema kuwa mripuko ulisikika uwanjani humo saa kumi na mbili na dakika 24 saa za china lakini hawakutoa taarifa zaidi.Kituo cha televisheni cha china Central kimesema katika mtandao wake kuwa mtuhumiwa aliejeruhiwa alikimbizwa hospitali baada ya kuripua bomu hilo na kuongeza kuwa usafiri wa ndege haujaathirika na hali ya kawaida imerejea katika uwanja huo.

No comments:

Post a Comment