Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, July 17, 2013

WAKILI ERASTO LUGENGE NUSURA AMUUE POLISI KWA RISASI MAENEO YA BOKO.


Gari la Wakili Erasto baada ya kugonga likiwa Kituo cha Polisi Wazo Hill.
Na Makongoro Oging'
ASKARI polisi wa usalama barabarani wa Kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam, Amani Leon amenusurika kuuawa kwa risasi na Wakili Erasto Lugenge wakati akipima ajali ya magari.
Tukio hilo lilitokea Julai 13, mwaka huu, saa 6.30 usiku Boko CCM, wilayani Kinondoni ambapo askari huyo alimtaka Lugenge wafike kituoni kutoa maelezo.
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kwamba Leon alipata taarifa kwamba Leon alipata taarifa kwamba kuna ajali imetokea maeneo ya Boko CCM ambapo alienda kutekeleza wajibu wake ikiwa ni pamoja kupima jinsi ajali ilivyotokea.
“Askari huyo alipofika eneo la tukio alikuta gari la Lugenge lenye namba za usajili T 181 DMM aina ya Mark II Grande limegonga kwa nyuma gari namba T 347 CAR Toyota Rav 4 lililokuwa likiendeshwa na James Mushi ambaye alimtaka Lugenge waende kituoni kutoa maelezo pia kupimwa kama alikuwa amelewa,” kilisema chanzo.
Kiliendea kudai kwamba gari la kuvuta magari ‘break down’ lilifika katika eneo hilo lakini Wakili Lugenge ambaye zamani alikuwa polisi mwenye cheo cha mkaguzi aligoma kwenda kituoni.NA GPL

...Gari la wakili kwa nyuma.

Imeelezwa kwamba vurumai ikaanza ambapo wote walidondoshana chini, Leon alimuona Lugenge akichomoa bastola kiunoni akitaka kumpiga risasi lakini aliwahi kumgonga mkono kisha bastola ikadondoka chini.
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba Leon aliiwahi ile silaha na kumwamuru Lugenge atii amri ambapo alinyosha mikono juu ila alikataa kwenda kituoni ndipo askari yule aliamuru gari livutwe hadi Kituo cha Polisi Wazo Hill na ile bastola akaikabidhi kituoni hapo.
Imeelezwa kwamba tayari Lugenge anashikiliwa kituoni hapo na Leon alikwenda kutibiwa katika Hospitali ya Mwananyamala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura alipoulizwa juu ya sakata hilo alikiri kuwepo.
“Lugenge tunamshikilia kwa upelelezi na wakati wowote tutamfikisha mahakamani tukimaliza uchunguzi wetu. Sikutegemea wakili kufanya kitendo hicho kibaya,” alisema Kamanda Wambura.

No comments:

Post a Comment