Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, September 4, 2013

Mwanamke akamatwa na madawa ya kulevya katika uwanja wa ndege mchana wa leo


 
 Mama mmoja  wa  kinigeria   amekamatwa na madawa ya  kulevya  mchana  huu  katika uwanja wa ndege wa JNIA  akijaribu  "kum-bypass "  Dr.Mwakyembe. 

Mwana  mama  huyo aliyetambuliwa  kwa  jina  la  Ojo Athnonie  alikuwa  amevaa   bai bui kwa juu na kufunika sura yake  yote.....

Taarifa  zinaarifu  kwamba  mama huyo alikuwa akienda na Ethiopian Airways na hivi sasa yuko  chini ya  ulinzi  mkali wa polisi .....
 
Kaimu kamanda wa polisi katika uwanja huo, Kamanda Renatus Chalia amesema raia huyo aliingia nchini tangu tarehe 30 mwezi wa nane mwaka huu kama mfanyabiashara wa viatu na mikoba. 
 
Mwanamke  huyo anadaiwa  kutumia  ubunifu  wa  ziada kwa  kanunua  powder za johnson kubwa na  kuzikata  kwa juu na  kisha  kuweka  kete  99  ambazo  zote  zimenaswa.CHANZO THECHOICE TZ

No comments:

Post a Comment