Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, September 15, 2013

Polisi Simiyu yatoa ripoti ukatili wa Dagashida, fisi wakoleza mauaji



Wananchi wa Simiyu wakiwa kwenye mkutano wa pamoja kujadili suluhisho la mauaji ya kikatili eneo lao 

Wiki iliyopita katika ukurasa huu, tuliwaletea mwendelezo wa ripoti maalumu kuhusu mauaji yaliyokuwa yakitekelezwa mkoani Simiyu kupitia Baraza la Kimila maarufu Dagashida na jinsi wananchi wanavyoogopa kutoa ushirikiano kwa polisi.
Leo tunaendelea na sehemu ya tatu na ya mwisho ya ripoti hiyo, pamoja na mambo mengine ikiainisha takwimu za vifo zilizotolewa na Jeshi la Polisi kutokana na matukio mbalimbali ya mauaji ya Dagashida.
Wanakijiji hawatoi ushirikiano
Kamanda Msangi anakiri kuwepo kwa changamoto ya kukosa ushirikiano kutoka kwa wananchi wakihofia usalama wao.
“Sisi tunawaomba wasiogope kutoa taarifa za ukatili huo, lakini pia tunaomba mashirika na dini waendelee kuelimisha,”anasema Kamanda Msangi.
Anaeleza kusikitishwa kwake na viongozi wa kisiasa kutoshiriki katika harakati za kukemea ukatili wa baraza hilo akifafanua tangu alipoanza kazi mkoani Simiyu hajawahi kuona wala kusikia mbunge yeyote wa mkoa huo akikemea ukatili wa Dagashida.
“Hakuna mbunge au diwani yeyote mwenye nguvu ya kuzuia baraza hilo kwa sababu wanalitumia kisiasa, kwa hivyo niwaombe waache kuchanganya siasa na maisha ya watu. Ni vyema wakashiriki kuelimisha,” anasema.
Polisi na takwimu za mauaji ya Dagashida
Takwimu za Jeshi la Polisi mkoani Simiyu zinaonyesha kuwa matukio ya mauaji hayo yanahusisha sababu mbalimbali ikiwamo kugombania mirathi, mipaka ya ardhi, imani za kishirikina pamoja na kujichukulia sheria mkononi.
Wiki iliyopita Mkuu wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi Salum Msangi alisema: “Nilipoingia Simiyu hali ilikuwa mbaya sana. Tulipokea ripoti za matukio kama hayo, hata ya watu watano kuuawa kwa siku, kuona hivyo kwa kushirikiana na mkuu wa mkoa tulizunguka Mkoa wa Simiyu wote kupiga marufuku uwepo wa baraza hilo…,”
Maelezo hayo ya Kamanda Msangi yalimaanisha kuwa katika kila siku saba za wiki watu 35 waliuawa mkoani Simiyu na katika mwezi mmoja wastani wa watu 150 waliuawa katika matukio yaliyohusisha kikundi cha Dagashida.
Hata hivyo, takwimu za jeshi hilo zilizotolewa wiki hii zinabainisha kwamba jumla ya watu 117 ameuawa katika vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Simiyu kati ya Juni 2012 hadi Juni 2013.na gazeti la mwananchi

No comments:

Post a Comment