Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, September 8, 2013

Tazama Picha Jinsi Kilimanjaro Music Tour 2013 Ilivyoacha Historia Kahama

  Linex akilishambulia jukwaa na wimbo wake wa Aifola
Kwa mara ya kwanza katika historia ya mji wa Kahama na vitongoji vyake, wakazi wake walipata nafasi ya kuwashuhudia wakali wa muziki zaidi ya 10 katika jukwaa moja katika tamasha la Kilimanjaro Music Tour 2013 lililofanyika katika uwanja wa taiga Kahama na kushuhudiwa na maelfu ya wakazi wa rika zote waliojitokeza na kuujaza uwanja wote.  Wakali hao Linex, Profesa Jay, Roma, Ben Pol, Fid. Q, Lady Jaydee, Izzo Bizness, Barnaba na Recho walilishambulia jukwaa kwa masaa sita mfululizo huku wakati mmoja wakipata nafasi ya kumuimbia Ben Pol wimbo wa Birthday kutokana na kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa usiku wa kuamkia Jumapili.



 Recho na madansa wake katika steji ya Kili Music Tour Kahama
  Shabiki mmoja alipata nafasi ya kucheza na Rech
  Kutoka backstage: Izzo Bizness, Alice, Fid Q, Kala Jeremiah na Ben Pol
 Ben Pol na Alice wakiimba wimbo wao mpya wa Waubani

 Ben Pol akiwaimbisha mashabiki kwa hisia
 Barnaba Boy jukwaani

Linex katika backstage ya Kili Music Tour
 Izzo Bishara, Izzo Bizness akiiwakilisha Mbeya mjini Kahama

  Izzo Bizness na Barnaba wakishambulia jukwaa kwa pamoja

 Baada ya kushuka jukwaani mashabiki hawakutaka kupoteza nafasi ya kupiga nae picha.

  Hip Hop ikiendelea kuwakilishwa na Kala Jeremiah
 Kala Jeremiah akiwauliza mashabiki kama wameilewa Kikwetu kwetu

 Jibu la mashabiki lilikuwa ni hili
 Roma Mkatoliki akiwarusha mashabiki waliofurika uwanja wa taifa Kahama
 Ma-DJ kazini kuhakikisha hakuna kinachoharibika
 Linex akiwa na wadau Shaaban Mpondela na Pius toka Frontline Novelli
  Lady Jaydee na Profesa Jay wakiimba Joto Hasira

 Profesa Jay akiifunga Kili Music Tour Kahama

 Mashabiki wakinyoosha mikono juu kuwashukuru wakali wa muziki waliopanda jukwaani

No comments:

Post a Comment