Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, November 20, 2013

GHANA HAOOOOOO KOMBE LA DUNIAAAAA


PRINCE_03b87.jpg
TIMU ya taifa ya Ghana, imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil, licha ya kufungwa mabao 2-1 na Misri katika mchezo uliomalizika muda mfupi uliopita kwenye Uwanja wa jeshi mjini Cairo.
Ghana imefuzu kwa ushindi wa jumla ya mabao 7-3, baada ya kufanya kazi nzuri katika mchezo wa kwanza mjini Kumasi mwezi uliopita na sasa watakwenda Brazil kujaribu kuendeleza mafanikio ya fainali zilizopita Afrika Kusini mwaka 2010 walipofika Robo Fainali.
GHANA_1158a.jpg
EGYPT_17e55.jpg
Misri, waliokuwa wakicheza nyumbani kwa mara ya kwanza mjini Cairo ndani ya miaka miwili, walianza vizuri na kuongoza kwa 2-0, mabao ya mshambuliaji wa Wigan Athletic, Amr Zaki na Gedo.
Lakini Kevin-Prince Boateng akaifungia Ghana bao la kufutia machozi dakika za lala salama na kufanya matokeo yawe 7-3, baada ya awali kushinda 6-1 nyumbani.
Ghana imeungana na timu nyingine tatu za Afrika kufuzu kwenye fainali hizo, Ivory Coast, Nigeria na Cameroon na mchezo kati ya wenyeji Algeria na wageni Burkina Fasso utakamilisha idadi ya timu tano zitakazoliwakilisha bara hili kwenye fainali hizo.
Katika mchezo wa kwanza, Burkina Faso ilishinda 3-2 nyumbani, maana yake Algeria hata wakishinda 1-0 leo nyumbani kwao, watafuzu pia.

No comments:

Post a Comment