Katibu
Mkuu Wizara ya Ardhi, Makazi,maji,Nishati na Madini Zanzibar Nd. Ali
Khalil Mirza na Mwenzake Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya utafiti na
uchimbaji wa Mafuta na Gesi Bwana Kamal Ahaya wakiweka saini mkataba
utakaotoa fursa kwa Wataalamu na Wahandisi wa Kampuni ya Ras Gas ya Ras
Al –Khaimah kufanya utafiti wa awali wa uwepo wa rasilmali ya mafuta na
Gesi Zanzibar.Wanaoshuhudia nyuma yao kutoka kulia ni Mfalme wa Ras Al –
Khaimah Sheikh Saud Bin Saqr Al – Qasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddipanoja na Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji
Nishati na Madini Mh. Ramadhani Abdulla Shaaban.
Katibu
Mkuu Wizara ya Ardhi, Makazi,maji,Nishati na Madini Zanzibar Nd. Ali
Khalil Mirza na Mwenzake Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya utafiti na
uchimbaji wa Mafuta na Gesi Bwana Kamal Ahaya wakiweka saini mkataba
utakaotoa fursa kwa Wataalamu na Wahandisi wa Kampuni ya Ras Gas ya Ras
Al –Khaimah kufanya utafiti wa awali wa uwepo wa rasilmali ya mafuta na
Gesi Zanzibar.Wanaoshuhudia nyuma yao kutoka kulia ni Mfalme wa Ras Al –
Khaimah Sheikh Saud Bin Saqr Al – Qasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddipanoja na Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji
Nishati na Madini Mh. Ramadhani Abdulla Shaaban.
Serikali
ya Ras Al – Khaimah na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimetiliana
saini mkataba utakaotoa fursa kwa Wataalamu na Wahandisi wa Kampuni ya
Kimataifa ya utafiti na uchimbaji wa mafuta na Gesi ya Ras Al –Khaimah {
Ras Gas } kufanya utafiti wa awali { SCAUT } katika maeneo ya ardhi na
Baharini ili kupata uhakika wa uwepo wa rasilmali ya mafuta na Gesi
Zanzibar.
Mkataba
huo umetiwa saini katika hafla maalum iliyofanyika katika Jumba la
Kifahari la Kifalme la Al -Dhait Palace Nchini Ras Al – Khaimah na
kushuhudiwa na Mfalme wa Nchi hiyo Sheikh Saud Bin Saqr Al – Qasmi na
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiuongoza
Ujumbe Mzito wa Mawaziri Saba wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kwa
Upande wa Zanzibar Saini hiyo imetiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi,
Makazi, Maji, Nishati na Madini Nd. Ali Khalil Mirza wakati ule wa Rais
Al – Khaimah imewekwa na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya utafiti na
uchimbaji wa Mafuta na Gesi ya { Ras Gas } Bwana Kamal Ahaya.

No comments:
Post a Comment