Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 30, 2014

MWILI WA SHEKH WA MKOA WA MARA WAWASILI UWANJA WA NDEGE MUSOMA

 NDEGE ILIYOBEBA MWILI WA MAREHEMU SHEKH ATHUMANI MAGEE

 MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPPA AKIELEKEA KWENYE NDEGE KUONGOZA WAOMBOLEZAJI

 RUBANI WA NDEGE AKIELEKEZA NAMNA YA KUTOA JENEZA LENYE MWILI WA MAREHEMU





 NDANI YA GARI MAALUMU LA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA(JWTZ)LILILOBEBA MWILI WA MAREHEMU

 WAUMUNI WA DINI YA KISSLAMU PAMOJA NA WANANCHI WA MJINI MUSOMA WAKIWA UWANJA WA NDEGE

 AFIDH WAZIRI MMOJA WA WATU WALIOTOKA NA MWILI WA SHEKH MAGEE DAR AKIAGANA NA RUBANI WA NDEGE



 MWILI UKIONDOLEWA UWANJA WA NDEGE TAYARI KUPELEKWA NYUMBANI



 MSAFARA WA MWILI WA SHEKH MAGEE UKIPELEKWA NYUMBANI



 MKUU WA MKOA WA MARA NYUMBANI KWA SHEKH

 MWILI UKISHUSHWA NYUMBANI

 WAOMBOLEZAJI WAKIWA NYUMBANI

MKUU wa mkoa wa Mara Mheshimiwa John Gabriel Tuppa ameongoza maelfu ya Wananchi wa Mji wa Musoma kupokea mwili wa Shekh wa Mkoa wa Mara Athumani Magee aliyefariki dunia usiku wa januari 28 katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Shekh Athumani Magee alifikwa na mauti baada ya kugua kwa muda na mrefu na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Bugando kwa muda kabla ya kuhamishiwa Muhimbili kwa uangalizi zaidi na akiwa njiani kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislam waliokuwepo kwenye uwanja wa ndege Musoma wakiusubili mwili wa shekh Magee wamesema  wamepata pigo kubwa kutokana na msiba huo kutokana na Shekh kuwa mstari wa mbele katika kuhimiza masuala ya dini.

Shekh wa mkoa wa Mara anatarajiwa kuzikwa kesho kabla ya swala ya adhuhur katika makabari ya Musoma Bus mjini Musoma.

   INNAH LILLAH WAINNAH ILLAH RAJIUUN

HABARI NA PICHA KWA HISANI YA SHOMARI BINDA

No comments:

Post a Comment