Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, January 30, 2014

RAIS BARACK OBAMA AMETUMIA HOTUBA YAKE YA KILA MWAKA KWA TAIFA KUELEZEA JINSI ATAKAVYOTUMIA MADARAKA YAKE KUJARIBU KUIMARISHA UCHUMI WA MAREKANI NA PIA KUKABILIANA NA BUNGE LA CONGRESS AMBALO LINA MGAWANYIKO.


Rais  Obama ameelezea mafanikio waliyonayo ikiwa ni pamoja na  kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira kwa kiwango kikubwa zaidi katika kipindi cha miaka mitano  kufufua   Sekta ya nyumba na makazi utengenezaji bidhaa  zinazobuni nafasi za ajira na kuzalisha mafuta zaidi ndani ya Nchi .
Aidha  Rais  Obama ameongeza kuwa licha ya kushuhudia miaka minne ya ukuaji wa uchumi na faida kubwa iliyovunwa na makampuni, ukosefu wa usawa umezidi kukita mizizi nchini marekani
Sanjari na hayo  ameongeza kuwa yupo tayari  kuendelea kufanyakazi na  wabunge wa  Bunge la Congress  ili kurekebisha baadhi ya mambo  lakini hatasita  kuchukua hatua za kurekebisha  mambo yanayotokea ndani ya bunge hilo hata bila  marekebisho ya sheria kupitia Congess.

No comments:

Post a Comment