Mbunge
wa Temeke Abbas Mtemvu akimkaribisha Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es
Salaam, Alhad Mussa Salum, alipowasili kwenye ukumbi, baada ya kuwalikwa
kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Jimbo hilo, ambao uliambatana na uchaguzi wa
Mwenyekiti wa Jimbo na Katibu ambapo katika jumla ya kura 54
zilizopigwa Ahmad Mnamala alipata kura 50 za ndiyo na tatu za hapana na
hivyo kuibuka mshindi, huku kwa jumla ya kura hizo hizo zilizopigwa,
Kasim Kiame akiibuka kuwa Katibu wa jimbo kwa kupata kura zote 54 za
ndiyo.

Sjeikh Salum akisalimiana na Mtangazaji wa Channel Ten, David Ramadhan

Shekh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,
akisalmiana na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temeke, Sikunjema Shabani,
baada ya kuwasili ukumbini.

Mtemvu, Sheikh Salum na Mwenyekiti wa CCM wilaya wakishangilia kabla ya kukaa vitini kuruhusu kikao kuanza

Wajumbe nao wakiwa wamesimama kuwalaki viongozi wa meza kuu

Meza ya ufundi ikiwa kazini kuhakikisha itifaki zote zinakwenda sawa

Sheikh Salum akizungumza mwanzoni mwa
mkutano huo ambapo alisisitiza msimamo wake kuwa yeye ni Muumin wa
serikali mbili na kuwataka wajumbe wa mkutano huo nao kuamini hivyo. Pia
aliwatakia uchaguzi mzuri wakimtanguliza Mungu mbele ili kumpata
kiongozi atakayelisaidia jimbo hilo la Temeke

Sheikh Salum akishikana mkono na Mtemvu baada ya kuzungumza

Mwenyekiti wa CCM wilaya aya Temeke akizungumza

Ahmad Mnamala akiomba kura kwa wajumbe wakati akijieleza

Kasim Kiame akiomba kura za kuwa katibu wa jimbo

Wajumbe wakigawiwa karatasi za kura


Baadhi ya wajumbe wakipiga kura.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO


No comments:
Post a Comment