Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Thursday, February 13, 2014

WAKAZI WA MTAA WA BAHIROAD MANISPAA YA DODOMA WAMEILALAKIA KAMATI YA ULINZI SHIRIKISHI KWA KUWACHANGISHA MICHANGO PASIPO KUONA UTENDAJI KAZI WAO .


Wakizungumza na Dodoma fm wakazi hao wamesema  wamekuwa wakitoa michango ya ulinzi lakini  hakuna utendaji kazi  wowote unaofanyika.Naye bwana  Amasha  Shaban mkazi wa mtaa huo ameitaka kamati ya ulinzi shirikishi kuweka ulinzi wa kutosha  mtaani hapo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa ulinzi shirikishi amekiri kuwepo kwa michango hiyo ambayo huwasaidia katika  matumizi mbalimbali ikiwemo kununua vifaa  kwa ajili ya kuimarisha ulinzi.Sanjari na hayo mwenyekiti ameeleza kuwa kuna changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo ikiwemo ujuzi mdogo katika suala la ulinzi.  

Viongozi wa kijiji cha solowu  wilayani   chamwino  Mkoani Dodoma  wameiomba  Serikali  kuwapelekea chakula cha msaada  kutokana na  njaa kukithiri  kijijini hapo.

Akizungumza na kituo hiki mwenyekiti wa kijiji  cha Solowu  bw. Omari  Salimu  amesema hali ya njaa kijijini  hapo ni kubwa  hivyo  inawafanya wakulima wengi washindwe kulima  mashamba yao  katika kipindi  hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

Nae afisa  Maendeleo wa kijiji hicho Bw Yohana Messai ameitaka serikali kupeleka  chakula cha bei rahisi ili kunusuru wimbi la njaa kijijini hapo.Kwa upende wake mkuu wa wilaya  ya Chamwino Bi  Fatma  Ally  amekiri kuwepo kwa upungu wa chakula  katika  baadhi ya vijiji  na hivyo amewataka  wakulama  kulima mazao yanayostahimili ukame.Na Dodoma Fm
 TUNAOMBA BOFYA HAPA NA ULIKE PAGE YETU KWA HABARI NYINGI MOTOMOTO(USIPITWEEEE)

No comments:

Post a Comment