Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, March 26, 2014

DARAJA LASOMBWA NA MAFURIKO MKOANI RUVUMA

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akiwa katika daraja la Chimate ambalo  mbao zake zimeoza na kupelekea kuhatarisha usalama wa  watumiaji wa  Daraja hilo katika Wilaya ya Nyasa. Ametoa agizo kwa Meneja wa TANROADS mkoani humo kubadili mbao katika daraja la Mto CHIMATE haraka  na kuweka kambi  katika daraja la Mto MBULI kufanya uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na wananchi ili kujua tabia ya mto huo hasa wakati wa masika.
Kutokana na Mvua kubwa zinazoelendelea kunyesha Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma  zimesababisha madhara makubwa katika vijiji viwili ndani ya wilaya hiyo  ikiwemo kuharibu mazao mashambani pamoja na kusombwa kwa daraja la mto  Mbuli katika kijiji cha Ng’ombo.Hali hii imepelekea wakazi hao  kupata tabu pale wanapougua huku wanafunzi wakishindwa kwenda shule kwa  muda wa mwezi mmoja na wengine mashamba yao kusombwa na maji.

Hali hiyo imepelekea huduma za kijamii kuwa ngumu kufanyika  ikiwa ni pamoja na upande wa matibabu pamoja na mahudhurio ya watoto shule.
Pichani aliyesimama katikati ni Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwangu akiwa katika Daraja la kijiji cha  MBUI ambacho daraja la mto ng’ombo limesombwa na  maji na kukigawa kijiji hicho sehemu mbili,  sehemu moja ikiwa inashule na sehemu moja  kukiwa na zahatari.
Pichani ni dereva wa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Ruvuma aliyejulikana kwa  jina moja la Komba akitoa msaada wa kuwavusha watoto wa shule katika  daraja la mto Mbuli ambalo nilamuda lililotengenezwa na wananchi wenyewe wa kijiji cha Ng’ombo.
Kulia ni mwenyekiti wa CCM Mh.Oddo Mwisho akiteta jambo na mkuu wa mkoa wa  Ruvuma Said Mwambungu kuhusiana na Daraja hilo lilisombwa na maji.
 Pichani ni wakazi wa Kijiji cha Ng'ombo wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Ruvuma  Said Mwambungu ambaye hayupo pichani akiwataka wakazi ho kuwa na subila  katika ujenzi wa daraja hilo kutokana na Mto huo kuwa na tabia za  kuhamahama. Hivyo akatoa agizo kwa wataalamu kuja na kuweka kambi ili  kujua namna ya kuweza kuudhibiti mto huo usijeukasababisha maafa tena  katika ujenzi huo pale utakapotengamaa.
Katika picha ni wakazi wa kijiji cha Ng'ombo wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa  Ruvuma ambaye hayupo katika picha huku wakiwa katika nyuso za majonzi  kutokana na mvua kusababisha uharibifu.(Picha zote na Demashones)

No comments:

Post a Comment