Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Sunday, March 2, 2014

MTANGAZAJI WA CHANEL TEN,SALUM MKAMBALA APATWA NA AJALI MBAYA MAENEO YA VIGWAZA.


Mtangazaji wa Channel  Salumu Mkambala, akipelekwa Theatre katika Hospitali ya Tumbi, Kibaha, Pwani.
Msanii wa kundi la Mizengwe, Hemed Maliyaga (wa kwanza kulia) akisaidiana na ndugu pamoja na mke wa Mkambala (wa tatu kushoto) kumpeleka mgonjwa Theatre.
...Mkambala akiingizwa Theatre.

STORI: DEOGRATIUS MONGELA
Baada ya Mtangazaji wa Channel  Salumu Mkambala kupata ajali na kugongana na lori akiwa safarini kuelekea Morogoro sababu za ajali hiyo zimetajwa.

Akizungumza na  mwandishi  wetu Hospitali ya Tumbi Kibaha, Pwani mdogo wa mtangazaji huyo, Ramadhani Mkambala alisema kaka yake alikuwa akielekea Morogoro na alipofika maeneo ya Vigwaza aligongana na lori alfajiri saa 10. 30  akiwa yeye na mtu mmoja aliyempa lifti.

Hata hivyo, chanzo cha ajali hiyo kilitajwa na Ramadhani kuwa ni kutokana na barabara ya eneo hilo kuwa na mashimo mengi hali iliyosababisha gari la kaka yake kuhama upande wake na kulivamia lori.

“Tulipopata taarifa tulishtuka sana lakini tunashukuru Mungu kuona kaka yangu yupo hai na amepata matibabu hapa Hospital ya Tumbi japokuwa ameumia mikononi na miguu na kuwekewa bendeji ngumu (POP) lakini tuna matumaini atapona na kuendelea na majukumu yake,” alisema Ramadhani.
HABARI KWA HISANI YA GPL


 

No comments:

Post a Comment