Huu ni mtaro wa kupitisha maji taka ambao umepita kati kati ya Hospitali ya Palestina amapo ulifumuka na kusababisha kusambaa kwa maji machafu katika kila kona ya Hospitali hiyo
Mmoja wa wagonjwa akiwa anangojea kupata huduma baada ya mvua hiyo kubwa kwisha
Haya ni maji machafu ambayo yametapakaa kila sehemu ya hospitali
Kushoto ni Mgonjwa akiwa amelala juu ya Benchi ambapo pembeni kuna maji na matope ambayo yamechanganyikana na kinyesi kutoka katika vyoo mbalimbali katika makazi ya watu.
Hii ndio hali halisi ya Chemba hii ambayo ipo ndani ya Hospitali ya Sinza Palestina
Hizi ni chemba zaidi ambazo zipo nje na pia zimeungana na zilizopo ndani ya Hospital hiyo
Wagonjwa zaidi wakingojea waganga kufika pia kumalizia kusafishwa kwa vyumba hivyo ili wapate hudumiwa
Moja ya Chumba ambacho kilikuwa kimejaa tope kikingojea kusafishwa
Hapa hata hapapitiki
Baadhi ya viti vikiwa vimeegeshwa kwa ajili ya kungoja kufanya usafi
Hakuna mtu katika maeneo haya kutokana na mvua kubwa iliyonyesha
Kila kitu kimekaa hovyo hovyo baada ya mvua kubwa hiyo kunyesha
Baadhi ya vifaa vya kutibia wagonjwa vikiwa juu ya moja ya kitanda cha kutibia wagonjwa huku watu wakingoja huduma ya matibabu.
Huu ndio Mtaro wa maji machafu ambao hupitisha maji,lakini wakati wa mvua kubwa ukishindwa kupokea maji yanaingia ndani ya Hospitali
Picha zote na Dar es salaam yetu

No comments:
Post a Comment