Mahakama ya Umoja wa Mataifa inyoshughulikia Mauaji ya Halaiki ya Rwanda (UN-ICTR) iliyo na makao yake makuu mjini Arusha leo imetoa msaada wa magari mawili ya kiusalama (Amoured Cars) kwa jeshi la polisi mkoani Arusha ili kuimarisha shughuli zake za kiusalama mkoani hapo. Magari hayo ni baadhi ya yale yliyokuwa yakitumika kwa shughuli za usalama - kubebea watuhumiwa au watu nyeti - na mahakama hiyo inyotarajiwa kumalisha shughuli zake mwakani. Magari hayo ni yale yaliyoimarishwa kiusalama ambapo hata risasi haziwezi kupenya kwenye bodi yake au kwenye kioo chake. Magari hayo yalikabidhiwa na Mkuu wa Idara ya Fedha na Kaimu Mkuu wa Utawala wa Mahakama hiyo Bw. Robert Foot kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo Afande Liberatus Sabas
BALOZI KAGANDA ASHIRIKI MDAHALO WA VIONGOZI WAANDAMIZI ZIMBABWE, AELEZA
MCHANGO WA TANZANIA KIKANDA
-
Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Kamishna wa Polisi (CP) Suzan Kaganda,
ameshiriki mdahalo wa viongozi waandamizi uliofanyika katika Chuo Kikuu cha
Zimb...
37 minutes ago

No comments:
Post a Comment