Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Monday, March 17, 2014

VIONGOZI WA BARCLAYS AFRICA WATEMBELEA TANZANIA


  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Africa, Kennedy Bungane (kushoto) akimsikiliza Balozi wa Malawi nchini, Bi.  Flossie Asekanao Gomile-Chidyaonga wakati wa mkutano uliondaliwa kwa wateja na wadau wakati viongozi wakuu wa Kundi la Barclays  Afrika (the Group),  wakitembelea nchini, jijini  Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni Ofisa Mkuu Vihatarishi (Risk) wa Barclays Afrika, Anil Hinduja.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Africa, Kennedy Bungane (kulia) akisalimiana Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Chemi & Cotex, Lakshmi Narayan wakati wa  mkutano uliondaliwa kwa wateja na wadau wakati viongozi wakuu wa Barclays  Afrika, wakitembelea jijini  Dar es Salaam. Katikati ni baadhi ya maofisa wa NBC, Daniel Kaila (wa pili kushoto) na Azza Ernest Mnzava.
  Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barclays Africa, Kennedy Bungane (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Huduma  Rejareja za Kibenki wa NBC, Mussa Jallow  katika mkutano uliondaliwa kwa wateja na wadau wakati viongozi wakuu wa  Barclays  Afrika, wakitembelea nchini.. Wengine kulia ni Mkurugenzi wa Bodi ya NBC, Dr Hussein Kassim na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Chemi & Cotex, Lakshmi Narayan.   
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Bi. Mizinga Melu (kushoto) akiwa na baadhi ya wageni waalikwa katika mkutano huo jijini Dar esd Salaam.
 Ofisa Mwendeshaji Mkuu wa NBC Tanzania, Maharage Chande (kulia), akisalimiana na  Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Nyanza Mines, Mukesh Mamlani  wakati wa mkutano huo  jijini  Dar es Salaam.  Katikati ni baadhi ya maofisa wa NBC, Godfrey Nderingo (wa pili kushoto) na Cletus Shirima. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Mizinga Melu (kushoto) akiwa na wageni wengine katika mkutano huo. Kundi la Barclays Afrika ‘the Group’, limetokana na kuunganishwa kwa Kundi la ABSA ya Afrika Kusini (ABSA Group Ltd) na sehemu kubwa ya shughuli za Benki ya Barclays barani Afrika hapo Juni 31, 2013. ABSA (sasa the Group) ikimiliki asilimia 55 ya hisa ndani ya NBC, serikali ya Tanzania asilimia 30  zinazobaki zikimilikiwa na mashirika ya fedha ya kimataifa

No comments:

Post a Comment