Social Icons

IMETOSHA

IMETOSHA

Wednesday, July 16, 2014

JAJI KADURI AJITOA KESI YA MAUAJI YAPROFESA JWANI MWAIKUSA


Jaji Lawrence Kaduri wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, amejitoa kusikiliza kesi ya mauaji ya watu watatu akiwemo aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Sheria, Profesa Jwani Mwaikusa (pichani).
Jaji Kaduri alijitoa katika kesi hiyo juzi wakati ilipotajwa kwa ajili ya kusikiliza ushahidi wa upande wa Jamhuri kwa siku nne mfululizo, akidai ana maslahi nayo.
Alisema hawezi kusikiliza kesi hiyo kwa kuwa alisoma na Profesa Mwaikusa na alikuwa naye kila mahali hivyo akisikiliza hawezi kutenda haki. Shauri hilo liliahirishwa hadi kipindi kingine kitakachopangwa.
Hii ni mara ya pili kwa majaji kujitoa katika kesi hiyo, ambapo Jaji Dk Fauz Twaib alijitoa kwa kuwa aliwahi kufanyakazi na Mwaikusa.
Washitakiwa katika kesi hiyo ni Joseph Machecho na Jackson Zebedayo, ambao wanadaiwa Julai 13, 2010, katika eneo ya Mbezi Salasala, mtaa wa Mkonde, Dar es Salaam kwa makusudi walimuua Profesa Mwaikusa, Gwamaka Daudi na John Mtui.
Washitakiwa hao walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mwaka 2010 na baada ya upelelezi kukamilika kesi ilihamishiwa Mahakama Kuu.

No comments:

Post a Comment